Bunge lapitisha Marekebisho Sheria nne za Kilimo
Bunge lapitisha Marekebisho Sheria nne za Kilimo
28 Aug, 2026
Bunge limepitisha Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria za Kilimo wa Mwaka 2026 (The Agricultural Laws Amendments Act, 2026) ambao unapendekeza marekebisho katika sheria nne. Muswada huo umepitishwa katika Kikao cha Pili cha Mkutano wa nne wa Bunge la 13, kilichofanyika tarehe 27 Agosti 2026, jijini Dodoma.
Sheria hizo ni Sheria ya Tasnia ya Mkonge, Sura ya 30; Sheria ya Usalama wa Chakula, Sura ya 249; Sheria ya Tasnia ya Sukari, Sura ya 251; na Sheria ya Tasnia ya Chai, Sura ya 275








